Education

ZANGU...

Hello Friends,Mamboz!!!!!!!!!!!!!!!!

My time is very limited jamani,yaani busy gal huku na huku elimu unaitaka kazi unaitaka bado hujaingia kwenye haya ma internet kujua kinchooendelea Dunian basi unajikuta uko Busy,

Najiandaa na UE exams right now.........but its my plaesure,just to see there are friends around me!!!Love you all my blog viewers...........


































Shule ina raha yakeee meeeeeeeeen!!!!!!!!!!!!!Nchi yenyewe ishauzwa najiandaaa Kutrade my citizenship somewhere else
















Click here to join nidokidos


Click here to join nidokidos 
Click here to join nidokidos 
''Never fight. 
Nothing is worth fighting for. 
Wisdom never fights, it waits patiently, speaks positively, 
releases easily, sees benefit in everything 
and envisions a future of abundance...
knowing that all needs will be met at the right moment, 
in the right way. 
If you think life is a struggle you will always be struggling,
If you think life is a breeze, 
your attitudes and actions will convey lightness and easiness. 
And that's what attracts everything you need, and much more. 
Make today a breeze not a battle.'' Innerspace
Try not to worry.
Try to look at what  you're going through as a challenge 
rather than an obstacle, a time to develop patience. 
To achieve more objectivity , detach yourself from the struggle.
Have confidence in yourself, and realize that you can change your 
attitude even if you can't change the circumstances.
Look closely at your troubles.
Don't let them cause you to give up.
Befriend them and learn from them.
Feel them lose their power over you.
Allow them to teach you what you want to know and move on..
Try not to be afraid.
You're a survivor. 
You're going to handle this.
You're going to find strength you didn't know you had 
and grace to deal with what ever comes along. 
Pretty soon , you'll be on the other side, and it's just  a matter of time until             
that even though the road was rocky, you persevered and carried on.

 

WAKAGUZI WA NDANI WAPATA MAFUNZO UA UKAGUZI

Baadhi ya wakaguzi wa ndani  kutoka Idara zinazojitegemea na Wizara mbalimbali wakiwa katika mafunzo ya siku nne ya kuwajengea uwezo wakaguzi hao juu ya kufanya ukaguzi unazingatia maeneo hatarisha ili kupunguza hoja za kikaguzi. Mafunzo hayo yalianza leo jijini Dar es salam na kufunguliwa na Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani Constantine Mashoko(hayupo pichani)
Picha  na Tiganya Vincent-MAELEZO- Dar es salaam
Baadhi ya wakaguzi wa ndani  kutoka Idara zinazojitegemea na Wizara mbalimbali wakiwa katika mafunzo ya siku nne ya kuwajengea uwezo wakaguzi hao juu ya kufanya ukaguzi unazingatia maeneo hatarisha ili kupunguza hoja za kikaguzi. Mafunzo hayo yalianza leo jijini Dar es salam na kufunguliwa na Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani Constantine Mashoko(hayupo pichani)
Mkaguzi Mkuu Msaidizi wa Ndani (Assistant Internal Auditor General ) Emmanuel Subi akieleza malengo ya mafunzo ya siku nne ya wakaguzi wa ndani kutoka Wizara mbalimbali na Idara zinazojitegemea  leo jijini Dar es salaam juu ya kuwajengea uwezo wakaguzi hao katika kufanya ukaguzi unaozingatia maeneo hatarisha ili kupunguza hoja za kikaguzi.
Kaimu Mkaguzi Mkuu wa Ndani Constantine Mashoko akifungua mafunzo ya siku nne ya wakaguzi wa ndani kutoka Wizara mbalimbali na Idara zinazojitegemea  leo jijini Dar es salaam juu ya kuwajengea uwezo wakaguzi hao katika kufanya ukaguzi unaozingatia maeneo hatarisha ili kupunguza hoja za kikaguzi.

 

Bi Mkora Alonga: Mwanamke Akikukubalia Haraka Si Kwamba Ni ' Mrahisi', Amekuzimia Muda Mrefu!

Na nyie kina kaka punguzeni kuchagua, kwa mfano huoni kuwa ni risk kuanza kutaka kufanya mapenzi na msichana mapema hii na kwa yule aliyesema kuwa wengine wanakubali kirahisi, sasa kwa nini umuombe tendo la ndoa?

 Kwanini usifanye urafiki wa kawaida kwanza bila kufanya mapenzi, mkazoeana mkajuana tabia kama ni wa dizaini ya kutaka mali au wa kujenga, kisha ndio mkaenda stage nyingine? Hivi ngoja leo niwape dillema mnayowatwisha kina dada.

Kwa mfano dada wa watu keshakaa wee miaka hatokei mtu wa kumuomba uchumba, mara leo hii umetokea wewe unamtaka urafiki na mara unatanguliza kuomba ngono, hapo anakuwa kwenye dillema, akikukatalia utaingia mitini kimoja na yeye kubaki mpweke. Sasa akupe ngono au abaki mpweke? Na pengine huko nyuma alishakutana na kina kaka maguberi yakataka ngono akakataa ana kaachwa solemba! Sasa hapo afanyeje akukubali umtose vile vile kwa kumuona yu rahisi au akukatalie a risk loneliness!

Kisha swali la kizushi, kama mtu umempenda kwa nini umtie hiyo mitihani ya kuanza kumuomba ngono? Ndio kujionyesha Urijali au? Na kwa kuwa umeomba mwenyewe kwa nini ukipewa uanze kuwa na mashaka kama si unafiki ni nini? Sasa ulikuwa unaomba ili ukataliwe? Na msichana akikukubalia haina maana kuwa ni mrahisi bali pengine amekuzimia muda ila ameshindwa kukwambia anasubiri golden chance na hiyo umeileta sasa afanyaje?

Cha msingi ni kuwa muwazi na mkweli.  Mweleze wazi mwenzako, kusiwe na unafiki, kama kuna mpango wa kuoana basi na muwe marafiki kama ni mpango wa kuchezeana basi na mwambie aanze mbele ili asikuzibie wengine wakafikiri una  mtu kumbe huna kitu! Lakini pia ukiwa bold wanaume wengine wanashangaa wanataka wao ndio waanze kutangaza ndoa!

 

WANYAMA WAKIWA BADO TUMBONI

 Hizi ni picha zilizotolewa na DOCUMENTARY MPYA YA NATIONAL GEOGRAPHIC ambazo uonesha
wanyama wakila tumbo kabla ya kuzaliwa,Petro Chinn anatumia compyuta na kamera katika utafiti huu




Unaweza kututumia picha na maelezo juu ya picha yako ili kuboresha na kusahidia katika uelimishaji lika

 

NIMR YAONGEA NA WANAHABARI KUHUSU RIPOTI YA UTAFITI WA CHANJO YA KANSA YA KIZAZI KWA MWANAMKE

Mkurugenzi wa Kuratibu na Kukuza Utafiti wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) Dkt. Julius Massaga(kulia) akitoa ufafanuzi leo jijini Dar es salaam kuhusu chanjo ya satarani ya shingo ya kizazi kwa wanawake wakati wa semina na waandishi wa habari.
 
                                             (Picha na Tiganya Vincent- MAELEZO- Dar es salam)
Mtafiti Mkuu wa Utafiti wa Chanjo ya kuzuia saratani ya njia ya kizazi  wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) tawi la Mwanza Dkt.Deborah Waston Jones(kushoto) akiongelea leo jijini Dar es salaam na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya utafiti wa mapokeo ya wananchi kuhusu chanjo ya saratani ya njia ya kizazi kwa wanawake . Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) tawi la Mwanza Dkt. John Changalucha(kulia)
Mkurugenzi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) tawi la Mwanza Dkt. John Changalucha(kulia)akiongelea leo jijini Dar es salaam na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya utafiti wa mapokeo ya wananchi kuhusu chanjo ya saratani ya njia ya kizazi kwa wanawake . Kushoto ni Mtafiti Mkuu wa Utafiti wa Chanjo ya kuzuia saratani ya njia ya kizazi  wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu(NIMR) tawi la Mwanza Dkt.Deborah Waston Jones

 

Wanaotaka Kusoma Marekani



  Tembelea link hapo chini
www.viu.edu

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA SOMO KUHUSU UZAZI WA MPANGO

Dr.Rose Madinda kutoka wizara ya Afya akitoa elimu kwa waandishi wa habari kuhusiana na uzazi wa mpango katika semina maalum kwa waandishi wa habari ilioandaliwa na wizara ya Afya kwa kushirikiana na Nyota ya kijani semina hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa DICC jijini Dar es Salaam hivi karibuni
(PICHA NA PHILEMON SOLOMON-FULLSHANGWE)
Mratibu wa uzazi wa mpango Bw;Deo Ng'wanansabi akitoa ufafanuzi katika semina hiyo.
Dr.Rose Madinda kutoka wizara ya Afya kushoto na Bi Marietha Haule kulia wakionyesha mchoro wa viungo vya mfumo wa uzazi wa mwanamke.
Msanii wa taarabu nchi Mzee Yusuph kutoka bendi ya Jahazi Morden Taarab akichangia mada katika semina hiyo
Baadhi ya waandishin wa habari wakiwa katika semina hiyo.

NI KATIKA MSIMU WA SIKUKUU YA PASAKA FOUR WAYS BUKOBA WANAKULETEA JINSI YA KUANDAA PILAU YA KUKU KWA AJIRI YA FAMILA YAKO.

Pilau Ya Kuku 

   




















Vipimo
Mchele wa basmati                                                3 vikombe
Kuku                                                                     ½
  Viazi                                                                      4
Vitunguu                                                                2
Thomu iliyosagwa                                                  2 vijiko vya supu
Binzari ya pilau nzima                                             1 Kijiko cha chakula
Binzari ya pilau                                                       ½ kijiko cha chai
Pilipili manga nzima                                                 ½ kijiko cha chai
Karafuu nzima                                                        8
Iliki nzima                                                               6
Mdalasini nzima                                                       5 vijiti
Pilipili mbichi iliyosagwa                                            2
Chumvi                                                                   kiasi
  Mafuta ya kupikia                                                    ¼ kikombe

 Namna Ya Kutayarisha Na Kupika:

1.     Osha mchele na roweka kwa muda kutegemea na aina ya mchele.
2.     Kata kuku vipande upendavyo, safisha kisha mchemshe kwa chumvi, pilipili iliyosagwa, thomu na tangawizi.
3.     Akiwiva kuku, mtoe weka kando, bakisha supu katika sufuria.
4.     Katika sufuria, kaanga vitunguu hadi vigeuke rangu ya hudhurungi.
5.     Tia thomu na tangawizi na binzari zote kaanga kidogo
6.     Kisha tia viazi kanga kidogo kisha tia kisha tia vipande vyako vya kuku na supu acha ichemke kidogo kisha tia maji ukisie kutokana na mchele unaotumia.
7.     mwisho tia mchele koroga uchanganye na vitu vyote acha ichemke kiasi kisha funika na punguza moto mpaka uive (huku ukiugeuzageuza)
8.     Ukishakuwa tayari pakua  kwenye sahani tayari kwa kula na salad na pilipili.

Unapoamua kupenda, vaa uvumilivu, ikibidi kubali kuwa bwege - 2


Wiki iliyopita katika makala haya nilieleza kwamba ni lazima uheshimu hisia za mwenzi wako. Ukiheshimu hisia za mwenzi wako na ukawa unajali za kwako, itakusaidia kukufanya uwe na tumaini chanya wakati wote.
Wakati wa matatizo, hasa kipindi ambacho hampo kwenye maelewano mazuri, utabaki na imani kwamba yote yatakwisha.
Penda kuamini kuwa “hili nalo litapita” kwamba wakati ambao mwenzi wako amenuna, hataki kuzungumza na wewe, unachopaswa kufanya ni kuheshimu hisia zake na uamini kwamba mwisho atatulia na uhusiano wenu utaendelea kwa maelewano makubwa.
Ukitaka kulazimisha awe mchangamfu kwako kipindi ambacho amenuna, ni sawa na kukaribisha matatizo zaidi. Ni vema kuelewana, watu wengi wanakosea katika uhusiano wao kwa sababu hawatumii busara ili kuwaelewa wenzi wao pindi wanapoonesha hali tofauti.
Busara iendelee kuchukua nafasi. Maneno “hili nalo litapita” liwe somo kwako. Kwamba leo umerudi nyumbani, umetaka chakula cha faragha, mwenzako amekwambia hajisikii vizuri. Hutakiwi kupandisha mizuka na kusababisha nyumbani pasilalike kwa siku hiyo.
Badala yake unapaswa kuvumilia. Jiulize mmefanya tendo mara ngani katika uhusiano wenu, iweje siku hiyo akwambie hajisikii? Ukilazimisha ni sawa na kumfanyia mwenzako ubakaji. Si ajabu akikuona unakuwa mkali, akakubali kukupa kwa shingo upande lakini si kwa ridhaa yake.
Mapenzi ni matamu lakini siyo rahisi kwa maana, nyakati nyingine utalazimika kuvumilia mambo ambayo pengine yakakuumiza. Mko wawili na kujenga tafsiri ya mwili mmoja. Pengine hata makundi yenu ya damu ni tofauti. Ilivyo maumbile yenu ni hasi na chanya ndiyo na damu zenu zilivyo.
Tofauti hiyo mnaielewa na kuikubali, iweje siku ukirudi nyumbani unamkuta amenuna na hataki kuzungumza na wewe ushindwe kuelewa? Hapo ndipo uvumilivu wako unahitajika. Ni kipindi ambacho busara zako zinapaswa kufanya kazi kwa asilimia 100. Usilazimishe afanye upendavyo wakali mwili wake haupo tayari.
Unaingia faragha na mwenzi wako. Ameshindwa kukuridhisha kabisa. Ni hekima zako kutambua kwamba siku hazilingani. Mbona siku nyingine alikupa mambo mazuri mpaka ukasema ‘poo’? Tatizo ni nini? Pengine nishati za mwili wake kwa siku hiyo hazipo sawasawa na hata yeye hajui.
Ukimkejeli kuwa hajiwezi ni sawa na kumchinjia baharini. Siku zinazokuja atashindwa kabisa. Si kwa sababu uwezo wake ni mdogo, la hasha! Maneno yako ya kejeli na dharau ndiyo yatakayoufanya moyo wake usinyae na kukuogopa ndani kwa ndani. Fikra zake zitashambuliwa na ugonjwa hatari.
Si ugonjwa unaosababishwa na kirusi, hapana. Ni gonjwa la maneno litakaloshambulia ubongo wake. Kila mara kabla ya kuingia mchezo atakuwa na maswali ya kujiuliza. ‘Sijui leo nitashindwa tena?’ ‘Nikishindwa itakuwaje?’ ‘Atanitukana tena?’ ‘Hivi mimi ni mgonjwa?’
Mwisho wa maswali hayo atahitimisha kauli kwa kusema: “Inawezekana mimi ni mgonjwa kweli ndiyo maana nashindwa kazi.” Amini kuwa kauli hiyo ndiyo ugonjwa hatari ambao utashambulia hisia zake na kuusababisha mwili ushindwe kufanya kazi sawasawa.
Ukitaka kuendelea kufurahia mapenzi ni vizuri umpe moyo mwenzi wako pale inapoonekana ameshindwa kutekeleza kazi ya faragha inavyotakiwa. Kaa naye vizuri na umueleze kwa lugha laini kwamba baadaye au siku inayofuata mtafanya tena kikamilifu na hakutakuwa na kushindwa.
Ikibidi msifie, mwambie kuwa yupo kamili kwa sababu kila siku mnapoingia kazini huwa unatosheka. Mueleze kuwa siku hiyo anasumbuliwa na uchovu au hajisikii vizuri. Maneno hayo utayaona kidogo lakini yatamjenga ipasavyo. Yatamrejeshea ari na afya, kwa hiyo siku nyingine hatakuogopa.
Mapenzi ni matamu lakini siyo rahisi. Hii imesababisha watu wengi kushindwa kushirikiana vema na wenzi wao. Jambo dogo la kumuelewesha mwenzake linakuwa tatizo mpaka uhusiano unageuka shubiri. Wawili walioitana majina matamu na yenye kupendeza, wanageuka maadui.
Wanatangaziana sifa mbaya. “Yule muoneni hivyo hivyo kwa nje, hajiwezi kabisa kitandani.” Ni maneno ambayo si mageni. Yanasababishwa na watu kutotambua thamani ya mapenzi, ugumu uliopo ili iwe rahisi kwao kupata alama A kwenye uhusiano wao. Mapenzi ni magumu lakini ni rahisi sana.
Kanuni ni moja tu, kuwa mwelewa. Unaona mwenzi wako anashindwa kukufikisha unapopataka, wewe una jukumu la kumwelewesha. Mfahamishe maeneo ambayo anatakiwa ayafanyie kazi ili ufurahie tendo. Amini kuwa ukifanya hivyo, itakuwa rahisi kwako. Mapenzi ni asali itulizayo moyo.

MAPISHI YA KEKI YA MAZIWA

Posted on 30.March 2012


Vipimo
Siagi                                                               Kikombe 1
Sukari                                                             Kikombe 1 (usijaze sana)
Unga                                                               Vikombe 2 (usijaze sana)
Maziwa                                                            Kikombe 1
Mayai                                                               6
Baking Powder                                                1 Kijiko cha supu
Arki rose                                                           kidogo
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1.                       Changanya sukari na siagi mpaka ichanganyike.
2.                       Mimina mayai na maziwa uchanganye vizuri.
3.                       Mimina Baking Powder kwenye unga na uchanganye vitu vyote pamoja na arki rose.
4.                       Endelea kuchanganya vizuri mpaka uhakikishe vimechanganyika vizuri (unaweza kufanya bila ya mashine)
5.                       Chukua trey ambayo haitojaa ukiimimina, ipake siagi na umimine mchanganyiko wako.
6.                       Ipike (Bake ) 300 Deg C
 NENDA NA HIIIIII!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Jitihada za hali na mali zinafanywa na wakili wa kimataifa, James Mwang’amba kuhakikisha mteja wake, Anointed anaachiliwa huru. Kesi ya ujambazi wa kutumia silaha na kumteka mtoto wa waziri mkuu iliyokuwa inamkabili sambamba na rafiki yake Muddy, imewakalia vibaya.
Mwang’amba akisaidiana na mke wa Anointed, Specioza, wanafuatilia na kufanikiwa kupata vielelezo vyote muhimu walivyoelekezwa na mahakama, ikiwa ni pamoja na vyeti vya daktari kuthibitisha kuwa Anointed alikuwa na matatizo ya kisaikolojia wakati akishiriki vitendo vile vya uhalifu, hati za vifo vya wazazi wa Anointed na vielelezo kuwa mke na mtoto wake walikuwa wamelazwa wakati matukio hayo yakitokea.
Gerezani nako mambo si shwari baada ya Anointed kukutana na Ford wakiwa kupasua mawe. Anataka kumpiga na nyundo kubwa kichwani. Upande wa pili, hali ya Hans aliyechomwa kisu na Specioza wakati akijaribu kumuingilia kimwili mwanamke huyo mrembo bila ridhaa yake, inazidi kuwa tete baada ya kubainika kuwa  kisu kilikata mishipa yake ya fahamu mgongoni. Daktari anaeleza kuwa atakaa siku nyingi bila kurejewa na fahamu.
Je, nini kitafuatia? SONGA NAYO…  

 “Mkamateni huyo, ataua… huyooo… huyoooo… atamuua mwenzake huyo!”
alisikika mfungwa mmoja akipaza sauti kuwaambia wenzake baada ya kumuona Anointed amenyanyua juu nyundo kubwa ya kupasulia mawe na kutaka kumpiga nayo Ford.
Kilichotokea ilikuwa ni kama muujiza kwani Ford akiwa haelewi chochote, aligeuka nyuma ndipo aliposhtuka kupita kiasi baada ya kuona Anointed anataka kumpiga na nyundo kubwa. Ndani ya sekunde chache aliruka kutoka pale alipokuwa amesimama na kuangukia pembeni, nyundo kubwa ikatua usawa wa pale alipokuwa.
Kila aliyeshuhudia tukio lile alishika kichwa kwani ni kweli Anointed alikuwa amedhamiria kuua. Licha ya kumkosa, bado hakukata tamaa, aliinua tena nyundo ile na kuanza kumkimbiza Ford. Wafungwa wakawa wanapiga mayowe kukusanyana ili kumdhibiti Anointed. Kazi haikuwa nyepesi kwani kila aliyetaka kumuamulia ugomvi ule alikuwa akimtishia nyundo.

Ford alizidi kutimua mbio kuelekea mahali walipokuwa askari magereza, kila alipogeuka nyuma, Anointed alikuwa karibu yake huku akiwa ameiinua nyundo kwa nguvu. Ilibidi askari magereza waingilie kati, wakamkamata Anointed na kumpokonya nyundo, Ford naye akakamatwa na kukalishwa chini. Bila hata kuuliza sababu ya kutaka kumpiga mwenzake, Anointed alianza kupigwa na wale askari polisi kama mpira wa kona. Mafunzo ya kareti aliyopitia akiwa shuleni, yalimsaidia kujikinga kwani vinginevyo wale askari magereza wangemjeruhi vibaya.

Baada ya kumpiga sana, wale askari magereza walimtoa Anointed eneo lile la kupasulia mawe, wakamrudisha gerezani ambapo alifungiwa peke yake. Ford naye ilibidi arejeshwe gerezani kwani wakati akimkimbia Anointed, alijigonga mguu kwenye jiwe kubwa na kusababisha kucha ya kigole gumba kutoka.
Wafungwa wengine walibaki wameduwaa kutokana na kile kilichotokea siku ile.
“Jamaa ana hasira mbaya yule, angemuua kweli Mzungu.”
“Inaonesha wana bifu kubwa sana hawa, bila Mzungu kutimua mbio angeshakuwa marehemu,” walisikika wafungwa wawili wakijadiliana.

Muddy alinyamaza kimya kama hajui lolote linaloendelea. Akajikausha na kuendelea na kazi aliyokuwa amepangiwa. Baada ya kuingizwa gerezani, Anointed aliendelea kutweta kwa hasira. Alijilaumu kwa kumkosa Ford lakini akajiapiza kuwa lazima ipo siku atalipiza kisasi kwa yote aliyomfanyia.

***
Unajua wewe ni mwanaume wa kipekee sana?”
“Kwa nini Specioza?”
“Naona muda mwingi unautumia kwa ajili ya kazi, unaonesha una moyo wa kweli wa kutaka kunisaidia ili mume wangu atolewe gerezani.”
“Huo ni wajibu wangu, wala usijali.”
“Mh! Kama watu wote Tanzania hii wangekuwa kama wewe, hakika tungefika mbali kimaendeleo,” alisema Specioza  huku akimtazama Mwang’amba kwa macho malegevu.”

Specioza na Mwang’amba waliendelea kuzungumza mambo mbalimbali, wakawa wanacheka na kufurahi mpaka usiku sana. Kwa kadiri walivyokuwa wanazidi kuongea ndivyo Mwang’amba alivyozidi kuzisoma hisia za Specioza. Hakuna jambo ambalo hakutaka litokee kama kukiuka maadili ya kazi yake kwa namna yoyote ile, akatulia akiwa na hamu ya kutaka kuona mwisho wake.
“Kwani wewe una watoto wangapi?”

“Sina mtoto, bado sijaoa.”
“Mh! Kwa nini hujaoa mpaka sasa wakati umri wako unakuruhusu?”
“Mipango yangu bado haijakamilika, mambo yakienda sawa nitaoa tu.”
“Mwanamke utakayemuoa atapata bahati kubwa sana.”
“Kwa nini?”

”Wewe ni mwanaume muwajibikaji na unayejitambua, naamini hata familia yako itakuwa bora,” alisema Specioza.
“Mh! Ahsante, tayari ni saa sita za usiku, kwa nini usiende kupumzika? Si unajua kesho tunatakiwa kwenda mahakamani?”
“Kwa hiyo umechoka kuongea na mimi?”

“Hapana… basi tuendelee kupiga stori,” alisema Mwang’amba.
“Unajua mi nampenda sana mume wangu ila kuendelea kwake kukaa gerezani kunaufanya moyo wangu kuanza kufa ganzi.”
“Mh! Kwa nini moyo ufe ganzi wakati ulishaapa kuwa naye katika shida na raha?”

“Ni kweli niliapa lakini si unajua na mimi ni binadamu, tena bado kijana na damu inachemka… nina mahitaji yangu ya muhimu ambayo lazima mume wangu awepo kunitimizia, akiwa mbali kama hivi napata shida sana.”
“Najua unavyojisikia, lakini kama ulishakula kiapo cha kumlindia mumeo heshima yake na kumpenda, hakuna kinachoweza kukubadilisha mawazo.”

Ilitimia saa saba za usiku Specioza akiwa bado ndani ya chumba cha Mwang’amba.
“Specioza,” aliita Mwang’amba.
“Abee!”
“Naomba uende kupumzika chumbani kwako, muda umeenda sana.”
“Noo! Siwezi kwenda mpaka ufanye nitakachokwambia.”

“Kitu gani?” Mwang’amba aliuliza harakaharaka, Specioza akainuka pale alipokuwa amekaa na kumsogelea Mwang’amba.
“Nataka uni... nataka tunanii…”
“Mbona sikuelewi Specioza, unataka nini?” aliuliza Mwang’amba kwa sauti kavu, Specioza alipoona hataki kumwelewa, aliamua kufanya kwa vitendo.

Alimvamia Mwang’amba mwilini na kumkumbatia kwa nguvu, akawa anahema juujuu kama mtu aliyekimbizwa umbali mrefu. Kutokana na joto la mwili wake, Mwang’amba alishindwa kuzizuia hisia zake, naye akaizungusha mikono yake taratibu na kukishika kiuno cha Specioza, wakawa wanatazamana machoni.

“Nakuomba Mwang’amba kwa leo tu, mwenzio nina hali mbaya,” alisema Specioza huku akianza kuvua ‘night dress’ aliyokuwa ameivaa. Mwang’amba hakumsubiri amalize, alimsaidia kisha na yeye akaanza kutoa za kwake, maandalizi ya safari ndefu yakaanza kufanywa huku kila mmoja akionesha dhahiri kuwa na uchu wa safari.

***
Alfajiri na mapema, Anointed alishtuka kutoka kwenye usingizi wa mang’amung’amu, akasimama na kuanza kujinyoosha mwili. Alikuwa akisikia maumivu sehemu mbalimbali katika mwili wake kufuatia kipigo alichokipata kutoka kwa askari magereza, alipojaribu kumpiga Ford kwa nyundo kubwa.
Kilichomfanya awahi kuamka kuliko siku zote ni kwa sababu siku hiyo ndiyo ambayo wakili wake alitakiwa kufikisha vielelezo vyote mahakamani kwa ajili ya utetezi. Kwa kipindi kifupi tu alichokaa gerezani, alikuwa ameyachoka mno maisha yale. Alitamani kuwa huru na aliamini hilo linawezekana hasa kutokana na kazi kubwa iliyokuwa inafanywa na wakili wake, Mwang’amba.

Baada ya kufanya mazoezi ya kuuweka mwili sawa mlemle ndani ya gereza, alikaa na kuanza kusubiri muda wa kupelekwa mahakamani. Ilipotimu saa moja za asubuhi, askari magereza waliingia mle ndani na kuanza kuwaita majina watuhumiwa ambao walitakiwa kupelekwa mahakamani. Anointed alikuwa mmoja kati yao sambamba na rafiki yake, Muddy.

Watuhumiwa walitolewa hadi nje, wakapakizwa kwenye karandinga la polisi na safari ya kuelekea Mahakama ya Kisutu ikaanza. Walipofikishwa huku wakiwa chini ya ulinzi mkali, walipelekwa moja kwa moja kwenye vyumba vya ndani vya mahakama, kila mmoja akawa anasubiri muda wa kesi yake kusomwa.

Kesi ya Anointed ilikuwa ya tatu kusomwa, akatolewa kule kwenye chumba maalum na kupandishwa kizimbani akiwa na mwenzake Muddy. Wakati hayo yakiendelea, Anointed alikuwa akipepesa macho huku na kule akitarajia kumuona mke wake pamoja na wakili Mwang’amba. Licha ya kutazama karibu kila kona ya mahakama, hakumuona mkewe wala wakili Mwang’amba, hali iliyoanza kumtia wasiwasi.

Mwendesha mashtaka wa serikali alisoma mashtaka yaliyokuwa yanamkabili Anointed na Muddy, na kama walivyokuwa wamekubaliana siku ya kwanza, wakili wake akaitwa ili kuonesha vithibitisho alivyoagizwa na mahakama. Licha ya jina la wakili Mwang’amba kutajwa zaidi ya mara tatu, hakutokea mahakamani pale.

Je, nini kitafuatia? Usikose Alhamisi ijayo kwenye Gazeti la Amani.

UANDISHI WA FILAMU NA MAIGIZO
JIFUNZE NAMNA YA KUANDIKA NA KUANDAA SCRIPTS
MUUNDO WA HADITH


KUJENGA HADITHI YAKO



Baada ya kulipata wazo kwa ajili ya Filamu na Muhusika wako mkuu anayeambatana na hilo wazo, ni muda sasa wa kulitumia hilo wazo na huyo Muhusika, ili kutengeneza hadithi yako ya ukweli kwa ajili ya Filamu.
Kitu kikubwa ambacho unatakiwa kuwa na hakika nacho ni kwamba “Wazo lako na Muhusika wako mkuu vyote vinauwezo wa kubeba Filamu yenye masaa mawili”, ili kuwa na hakika na hili,jiulize kama Hadithi ina mvuto na Muhusika Mkuu pia kama ana kuvutia. kama utakuwa umefanya upembuzi kidogo,hakika jibu lako litakuwa “Hapana”. Hadithi yenye Mvuto na Muhusika mwenye Mvuto vyote vinagharama, na ili kutimiza ni lazima kufanya utafiti kabla ya kuingia kazini.
Jitahidi kuepuka kuandika script ya matukia yanayotokea sasa hivi, isipokuwa kama unamaelezo tosa ya kuhusu hilo tukio na namna ya kuifanya iwe na mvuto, Maproducer wengi wa Hollywood na Bollywood huwa hawapendi kutengeneza Filamu zinazohusu matukio ya sasa. Hii ni ndiyo maana filamu katika Hollywood na Bollywood inaandikwa,kuzalishwa na kupangwa kuzalishwa baada ya tukio kufikisha mwaka mmoja au miwili, huu ni Muda mzuri wa kufanya utafiti, Tambua kwamba Tukio la jana haliwezi kuuzika, kwamaana halina utafiti.
Na uhakikishe kwamba Hadithi yako inatazamika na kusukumika katika jamii. Kama unataka kuandika kuhusu Muhusika ambaye hadithi nyingi husimuliwa kumuhusu, basi kifaa muhimu ni kitabu (Novel), Mara nyingi Hadithi inayouzika katika Filamu ni zile zinazo simulika katika jamii, ambazo zinasimuliwa katika magazeti na Vitabu, na kama unataka Wingi huo kuhusu Muhusika basi jibu lako ni Kitabu cha hadithi (Noval), ongea na waandishi wa Vitabu pata kibali kwao au ongea na waandishi wa Mikasa katika Magazeti upatane nao, hadithi hizi huwa zina uzika sana, kwamaana bado zipo midomoni mwa jamii, unaweza pia kutengeneza hadithi kwa kutumia vitabu ambavyo vinatumiwa kufundishia Mashuleni, wanafunzi wengi ni wavivu kusoma vitabu, lakini kama ingekuwepo movie nadhani ingetumika ata madarasani, kama ilivyo nchi kama marekani na Uingereza, wanatumia mwanya wa elimu, kutengeneza filamu, na filamu zinatumika mashuleni kufundishia sambamba na Vitabu, na pia unaweza kutumiaa hadithi za watoto zinazosimuliwa kila siku majumbani kwao au mashuleni.Kama unataka hadithi yenye maongezi Mengi kuliko matendo basi maigizo ya majukwaani yanakufaa na kama ni maongezi tu maigizo ya redioni yanakufaa. Ila kumbuka Filamu si redio lazima pawepo na Matendo. Maigizo mara nyingi husimulika sana, kwahiyo ukiongea na wale wanaohusika unaweza kuongeza hadithi na kuiweka katika Mfumo wa filamu.
Ili kujenga Hadithi, Jitahidi kushika yafuatayo,yaliyopo ndani ya;
  1. Hadithi yenyewe
Kama nilivyojadiri katika somo la jana “Kujenga kipande cha uigizaji chenye Mvuto”, unatakiwa kuanza hadithi yako kwa mshindo, ili kuwavuta wasomaji katika filamu,yaani kumfanya Mtazamaji au msomaji atoke kwenye kiti aingie kwenye Movie. Kama hadithi yako inaanza huku Muhusika akitoka nyumbani kwake na kumtembelea rafiki na kisha kwenda benki ambapo ambapo anakutana na Majambazi, huu mlolongo wote unachosha haraka, unaweza kuondoa vipande na kuanza moja kwa moja benti ambapo kuna ujambazi, watazamaji wataghahiri kila kitu na kuonesha kujari. Unachotakiwa ni kumfanya Mtazamaji haone kwamba Muda ni mdogo na kumfanya haghahiri kila kitu.
Unatakiwa kuhakikisha kwamba hadithi inatokea katika eneo linalotambulika (recognisable location). Hata kama unaandika Filamu za vitu visivyo hasilia (Sci-fi),kuna namna ya kutimiza hili. Unakuwa na jengo linalofahamika lakini unalibadirisha lionekane kuwa ni lenye viwango vikubwa au vidogo kwa kikipindi kijacho, unaweza kufanya hivi kwa mji, madaraja n.k. Mfano, Jiji la Dar-es-salaam halina daraja la kuingia Zanzibar, lakini kama filamu yako itakuwa imelenga miaka 25 au 50 ijayo unaweza kutengeneza hadithi, inayoonesha daraja lipo, filamu hizi huitwa “Sci-fi”, unaweza kuchukua jengo maarufu na kulipamba au kulipunguza viwango, unaweza kulifanya jiji la Dar-es-salaam baada ya Miaka 50, kuwa jangwa au ni Magofu tu ndani yake huku majengo yanayofahamika yakionekana yalivyo haribika, Filamu za namna hii huwazina soko sana, haswa kama wahusika watatambua mazingira. Hii ndiyo sababu Marekani,filamu nyingi huigizwa kwa kutumia Mazingira ya jiji la New York, kwamaana hutambulika takribani ulimwengu mzima, kuliko miji mingine.
Hakikisha kwamba Unajisikia kuipenda hadithi unayoisimulia. Hii ndiyo maana kunamsemo wa kale unaosema “Jambo usilo lijua, ni usiku wa giza nene”, kama unapendelea kucheza Mpira wa Miguu na kutazama vipindi vya Vichekesho, basi itakuwa ni rahisi kwako kuandika Filamu ya vichekesho kuhusu Mpira wa Miguu, kuliko maisha ya kawaida (Drama). Kuna kipindi ambacho humtokea Mwandishi yeyote wa Script kama hicho anacho kiandika hakipendi, ambacho ni “Ugumu wa kuandika kurasa inayofuata ya script”, Tambua kile unachokipenda ndicho kitakacho kuwezesha kumaliza Script nzima.
Kitu kikubwa kukifikiria ni “Mafumbo”. Unatakiwa kufumbua mafumbo yaliyopo katika Filamu kinyume na hapo filamu itakuwa ni ngumu kuiamini, na ngumu kujihusisha. Kama chochote katika Filamu yako si cha kuaminika kwako, basi itaonekana kejeri mbele za watazamaji.
  1. Kwa kiwango gani Muhusika wako anahusiana na Hadithi
Muhusika jasiri ni yule ambaye,watazamaji wanaweza kujifunza kutoka kwake. Unatimiza haya kwa kumrushia Muhusika Matukio ya kutisha na Vikwazo vizito. Maisha ya Muhusika yanatakiwa kuwa magumu kiasi ambacho watazaji wamuhurumie na kwa huruma wakitaka Muhusika afanikiwe
Mbele ya Maisha ya Muhusika kuna dhahabu ndiyo maana inambidi kupitia Mazito. Lakini kama Muhusika wako atapitia katika shimo la kuzimu na kupata tirion 5, harafu akazipoteza basi Muhusika wako ni Mjinga. Kama unaona kwamba Lengo la Muhusika wako ni dogo sana basi kuna mambo mawili ya kufanya. Unaweza kumpa lengo kubwa au kumrejesha katika eneo ambalo anatimiza hilo lengo.
Kitu moja ambacho ni cha hakika, ni kwamba mwishoni Muhusika wako atapata mabadiriko. Kila alichopitia lazima kitambadirisha, Atatimiza lengo na pia kukua kiakili na kimawazo,kimwili ikiwezekana hata kiroho, hii ni kulingana na Budget ya Filamu. Muhusika anapoanza safari, anaweza akajiona ana ufahamu lakini katika safari atajifunza ni mchoyo, si mwenye huruma na mwishowe atajifunza kuwapenda wengine na hapo hapo lengo lake kuu likiwa limetimia.
Kama wewe ni mara yako ya kwanza kuandika script au kuanza safari ukiwa kama mwandishi wa script, ni vigumu sana kupata bajeti kubwa ili kuandika script kubwa, kwahiyo baada ya Kuandika script jitahidi, kuziweka vizuri zile scene ambazo zinakula fedha nyingi na kuziweka katika kiwango cha kawaida, njia nzuri ya kufanya hivi ni kuondoa Eneo lenye gharama, Mfano umeandika Location, kuwa ni BOT bank, hii ni gharama, Zile filamu zote unazoziona zinarekodiwa Kwenye benki kuna gharama, na kama hawatoenda benki basi watakodi jengo na kuligeuza kuwa benki haswa kama itahusisha Uharibifu, kwahiyo andika script ukiangalia ni nani atakaye itengenezea Filamu. Muhusika si lazima atembee kwenye gari yenye mirango sita ili kutimiza lengo, anaweza kuishi kijijini huku akiendesha baiskeli na akafikia lengo lake bila ata kufika mjini, Filamu yenye bajeti ya milioni 100 ina mambo mengi ya gharama kuliko ile ya milioni 5, na yote yanawezekana ata Filamu ya bajeti ya millioni 1 ipo.
Ijenge hadithi yako vizuri, ni msingi wa Filamu yako
Endelea kutufuatia