Saturday, September 8, 2012

MREMBO WA REDDS MISS ILALA APATIKANA



Miss Ilala 2012, Noela Michael (katikati), akiwa kwenye pozi na mshindi namba mbili Magdalena Roy Munisi (kulia), na mshindi namba tatu Mary Chizi muda mfupi baada ya kutangazwa washindi.
Miss Ilala aliyeachia taji hilo Salha Israel, akikatiza kuaga jukwaani hapo kabla ya kukabidhi rasmi taji hilo.
Mary Chizi akionyesha kipaji chake cha ziada wakati wa kugombea miss Talent ambapo aliibuka kidedea.
Magdalena Roy Munisi akicheza kama msanii wa Marekani … kwenye mchakato wa kugombea taji la kipaji.
Warembo walioingia kwenye tano bora ya shindano hilo.
Baadhi ya majaji waliyokuwa wakiratibu shindano hilo.
Msanii wa kundi la Wanaume Family Chege, akitumbuiza jukwaani hapo.
Wasanii wa filamu Bongo, Jacqueline Wolper (kulia), na Jennifer Kyaka ‘Odama’, wakifuatilia mpambano huo.
Vicent Kigosi ‘Ray’ (kulia), na Single Mtambalike ‘Richie’, wakifuatilia burudani hiyo.
Mtangazaji wa Times FM, Gardina G Habash (katikati), akiwa kwenye pozi na wasanii wa muziki wa kizazi kipya Bongo, Chege na Chid Benzi.
Mratibu wa mashindano hayo Gardina G, akiongea jambo mahari hapo.
Moja ya kikundi cha sanaa kikitumbuiza.
Baadhi ya Mashabiki waliyohudhuria mahari hapo wakifuatilia kwa makini burudani za mashindano hayo.
Usiku wa kuamkia leo kulifanyika mashindano ya kumsaka mrimbwende wa kuwakilisha Wilaya ya Ilala Ndani ya Ukumbi wa Nyumbani Lounge jijini Dar es Salaam, ambapo shindano hilo lilikuwa likishirikisha warembo 12.
Shindano hilo lililo anza majira ya saa nne na nusu usiku, lilipambwa na burudani kutoka katika bendi ya B Band, msanii wa TMK Family Chege na wasanii wa kusheki.
Hadi mwisho wa shindano hilo Noel Michael aliibuka kidedea, huku nafasi ya pili ikitua kwa Magdalena Roy Munisi na nafasi ya tatu ikitwaliwa na Mary Chizi ambaye pia amechukua taji la Miss mwenye kipaji akiwabwaga wenzake watano.
Habari/Picha: Musa Mateja/GP

No comments: