Friday, July 6, 2012

Sabodo Achangia M4C - CHADEMA


Mfanyabiashara maarufu na Kada wa CCM, Mzee Mustafa Jaffer Sabodo akikabidhi hundi ya Sh10m kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod Slaa nyumbani kwa Upanga, Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa CHADEMA, Antony Komu. Fedha hizo ilikuwa sehemu ya mchango mwingine wa Mzee Sabodo pamoja na ahadi kwa ajili ya kusaidia shughuli za chama hicho kuendelea kufanya kazi zake za kuimarisha na kueneza mtandao wake, ngazi za mitaa na vitongoji nchi nzima.

Dkt. Slaa akipeana mkono na Sabodo.

No comments: