Sunday, September 2, 2012

Majambazi Wateka Gari Na Kujeruhi Abiria Kibondo.

Na Juventus Juvenary wa Mjengwablog, Kibondo

Watu watatu wamelazwa katika Hospitali ya wilaya ya Kibondo Mkoani Kigoma wakitibiwa majeraha ya Risasi

Tukio hilo linafuatia watu wanaosadikiwa kuwa majambazi waliovamia Gari walilokuwa wakisafiria na kulishambulia kwa risasi zilizowajeruhi  sehemu mbali mbali za miili yao

Waliojeruhiwa ni Josephat Maimu miaka 31, Shukuru Benet 25 na Noel Godfrey 21 ambao walikuwa Safarini kutoka Kibondo-Kigoma kuelekea Kahama-Shinyanga katika shughuli zao za kawaida.

No comments: