Wednesday, August 20, 2014

Kikosi cha wapiganaji wa kiislam wenye msimamo mkali Islamic State kimeachilia video inayoonesha mauaji ya mwandishi habari mwenye asili ya Marekani aliyetekwa nyara nchini Syria 2012.


James Foley alipotea tangu alipokamatwa mateka na kushikiliwa nchini Syria yapata miaka miwili iliyopita.
Katika video hiyo mwandishi huyo wa kujitegemea anaonekana kuuawa na mtu anayemruhusu kutoa semi yake ya mwisho.
Foley ambaye katika video hiyo amevalia magwanda ya rangi ya chungwa akiwa amepiga magoti anasikika akisema kuwa ''Ninawaomba ndugu jamaa na marafiki wangu wasimame na kuzuia adui wangu Serikali ya Marekani kwa ukatili wanaoendelea kutekeleza ndani ya Iraq.''
Mpiganaji mmoja wa kundi hilo akizungumza kwa kizungu anailaumu Marekani kwa kifo cha mwandishi habari huyo.
''Kila siku mnaposhambulia jamhuri ya kiislamu manadhuru maisha ya muislamu na hivyo tunachukua maisha yetu ili iwe onyo kwako (rais) Obama''
Bofya hapa kuona vidio https://www.youtube.com/watch?v=RvGePlNavNs

No comments: