Habariz zote za Bunge na Benedict Liwenga-Maelezo, Dodoma. 
 | 
Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika inatarajia kutumia jumla ya shilingi 328,134,608,000/- katika mwaka ujao wa fedha.
Takwimu
 hizo zimetolewa leo mjini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Chakula na 
Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza wakati akiwasilisha Bungeni 
Makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara hiyo kwa mwaka 2013/14.
Alisema
 kuwa kati ya fedha hizo, Shilingi 247,094,320,000 ni kwa ajili ya 
Matumizi ya kawaida na Shilingi 81,040,288,000 ni kwa ajili ya Matumizi 
ya maendeleo.
Chiza aliongeza kuwa  Shilingi 210,175,943,000 ni kwa ajili ya Matumizi Mengine (OC) kwa ajili ya Wizara hiyo .
Aidha
 ,shilingi 25,602,969,000 ni kwa ajili ya Mishahara (PE) ya Wizara na 
Shilingi11,315,408,000 ni Mishahara (PE) ya Bodi na Taasisi zote 
zilizoko chini ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika.
Kwa
 upande shughuli za maendeleo, Chiza alisema kuwa Wizara hiyo imetenga 
kiasi cha shilingi 23,927,000,000 ikiwa ni fedha za ndani na 
shilingi 57,113, 288,000 ni fedha za Nje.
Wabunge
 wanatarajia kujadili bajeti ya Wizara ya Kilimo , Chakula na Ushirika 
kwa kipindi cha siku mbili ambapo itahitimishwa kesho.
Katika
 hatua nyingine Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Mhe. Chiza amesema
 Serikali inatarajia kufufua Kituo cha Kilimo Anga ili kukiwezesha kuwa 
na ndege na Wataalam watakaosaidia kudhibiti milipuko ya visumbufu vya 
mazao hasa Nzige.
Mhe.
 Chiza amesema kwa kiasi kikubwa Serikali imekuwa ikitegemea huduma ya 
ndege kukodi kutoka kwenye mashirika ya kikanda ya kudhibiti nzige 
wekundu na nzige wa jangwani ambazo wakati mwingine hazipatikani wakati 
zinazohitajika.
Kufuatia
 hali hiyo amesema Wizara katika mwaka wa fedha 2012/13 imekamilisha 
viwango vya kiufundi (Technical Specifications) kwa ajili ya kutangaza 
zabuni ya ununuzi wa ndege moja ya kunyunyuzia viuatilifu.
*******   *******
SERIKALI ITAENDELEA KUWAENDELE ZA WACHIMBAJI WADOGO WADOGO NCHINI
SERIKALI
 inatekeleza mkakati wa kuwaendeleza wachimbaji wadogo wadogo wa madini 
nchini kwa kuwatambua wao na mahitaji  ya mitaji na vifaa ili kutekeleza
 kazi yao kwa ufanisi.
Kauli
 hiyo imetolew na Naibu Waziri wa Nishati na Madini Stephen Julius 
Masele wakati akijibu swali na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini 
Stephen Ngonyani leo mjini Dadoma aliyetaka kujua ni lini wachimbaji 
wadogo wadogo wa Ng’ombeni, Kalalami, Kigwase watatambuliwa na Serikali 
na kupewa kipaumbele kwenye uchimbaji, na kupewa mikopo ya kujikimu 
wakati wakitafuta Madini.
Amesema
 kuwa katika kutambua umuhimu wa wachimbaji wadogo wadogo Wizara hiyo 
imeshakwishatoa imetoa jumla ya viwanja 612 vya uchimbaji mdogo wa 
madini katika maeneo ya Ng’ombeni, Kalalani na Kigwase ikiwa ni hekta 
3,864. 
Aidha,
 Naibu Waziri huyo ameongeza kuwa Serikali kupitia Shirika la Madini la 
Taifa na Wakala wa Jiolojia inaendelea kubainisha maeneo yanayofaa kwa 
uchimbaji mdogo ili yaweze kutengwa kisheria na kugawiwa kwa wachimbaji 
hao.
Masele
 alisema kuwa katika utekelezaji wa mkakati huo unashirikisha wachimbaji
 wenyewe kwa kuimarisha vyama vyao vya kimkoa na chama cha kitaifa 
(FEMATA) na kujadili masuala yao katika vikao vya pamoja vya kila baada 
ya miezi sita baina ya wawakilishi wao na Wizara.
Ameongeza
 kuwa Wizara ya Nishati na Madini inakamilisha taratibu za Mfuko rasmi 
wa kuwaendeleza wachimbaji wadogo ili kuwawezesha kupata mikopo ya vifaa
 vya uchimbaji wenye tija.
Aidha
 , Naibu Waziri huyo amewasisitiza wachimbaji wadogo wadogo kuwa mikopo 
hiyo wanayopata inapaswa itumike vizuri katika malengo waliyoombea ili 
wajihakikishie kuzalisha madini mengi na kujiongezea kipato.
*******   ********
UDHIBITI WA VISUMBUFU VYA MAZAO
SERIKALI
 itafufua kituo cha Kilimo Anga kwa kukiwezesha kuwa na ndege na 
Wataalam ili kujenga uwezo wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Masoko 
kudhibiti milipuko ya visumbufu vya mazao hasa Nzige.
Hayo
 yameelezwa na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi 
Christopher Chiza wakati akiwasilisha Bungeni Makadilio ya mapato na 
matumizi ya Wizara hiyo leo.
Mhe.
 Chiza amesema kwa kiasi kikubwa Serikali imekuwa ikitegemea huduma ya 
ndege kutoka kwenye mashirika ya kikanda ya kudhibiti nzige wekundu na 
nzige wa jangwani ambazo wakati mwingine hazipatikani wakati 
zinazohitajika hali ambayo husababisha Wizara kutegemea kukodisha ndege 
kutoka sehemu nyingine.
Amesema
 Wizara katika mwaka wa fedha 2012/13 imekamilisha viwango vya kiufundi 
(Technical Specifications) kwa ajili ya kutangaza zabuni ya ununuzi wa 
ndege moja ya kunyunyuzia viuatilifu.
Aidha,
 Wizara itaweka utaratibu wa kuingia ubia na makampuni binafsi na 
taasisi zinazotoa huduma kama hizo ili kukijengea uwezo kituo cha Kilimo
 Anga.
Wakati
 huo huo, Wizara ya Kilimo, Ushirika na Chakula ilisambaza lita ,6000 za
 kiuatilifu cha kudhibiti milipuko ya viwavijeshi katika mikoa ya Rukwa,
 Katavi, Mbeya, Tabora, Shinyanga, Mwanza, Geita. Dodoma, Morogoro na 
Tanga kunusuru hekta 16,418 za mazao ya nafaka.
******    *******
SERIKALI IMEFANIKIW A KUONGEZA WATAALAM WA KILIMO NCHINI HADI KUFIKIA 7,974
Wataalam
 wa ugani wameongezeka kutoka 3,379 waliokuwepo mwaka 2007 hadi kufikia 
7,974 mwezi Juni jana(2012) baada ya Serikali kuajiri wahitimu kutoka 
vyuo mbalimbali nchini.
Hayo
 yamesemwa leo mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na 
Ushirika, Mhe. Adam Kighoma Malima wakati akijibu swali Mhe. Mch. Dk. 
Getrude Rwakatare (Viti Maalum kupitia Chama cha Mapinduzi).
Amesema
 kuwa mwaka 2007 Serikali ilifanya tathmini ya upatikanaji wa huduma za 
ugani nchini na kubaini kwamba mojawapo ya vikwazo vikubwa vya 
upatikanaji wa huduma za ugani kwa ufanisi nchini ni upungufu mkubwa wa 
wataalam.
Malima
 ameongeza kuwa matokeo ya tathmini hiyo yalionyesha kuwa kulikuwepo na 
wataalam 3,379 nchini ikilinganishwa na mahitaji halisi ya wataalam 
15,082.
Amesema
 katika kukabiliana na changamoto hiyo , Serikali ilianza kutekeleza 
Mpango wa kuimarisha huduma za Ugani nchini ambapo kuanzia mwaka 2007 
Serikali imevifufua vyuo 13 vya kilimo nchini (MATIs) vilivyo chini ya 
Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika.
 “Ukarabati
 mkubwa wa vyuo vitatu MATI Ukiriguru, Maruku na Naliendele-Mtwara na 
ukarabati mdogo kwa baadhi ya vyuo kumi vingine umefanyika”. Mhe. Malima
 alisema.
Aidha,
 Mhe. Malima amesema kuwa vyuo viwili vya mashirika yasiyo ya kiserikali
 vilishirikishwa katika kutoa mafunzo yaliyolenga kuongeza idadi ya 
wataalam wa Ugani na vyuo hivo kwa sasa vina uwezo wa kudahili wanafunzi
 3,500 kwa wakati mmoja ikilinganishwa na uwezo wa kudahili wanafunzi 
600 uliokuwepo kabla ya mwaka 2007.

No comments:
Post a Comment