Friday, October 26, 2012

MSAMBATAVANGU ATOA SOMO KWA WAHITIMU CHUO KIKUU TUMAINI IRINGA


 Jesca Msambatavangu akionge na wahitimu wa chuo kikuu cha Tumaini Iringa
 Baadhi ya wahitimu
 Deputy Provost of Academic Afairs (katikati) Dkt Richard Lubawa


Mwenyekiti wa Chama cha Mapindunzi (CCM) na mkurugenzi wa Star International Jesca Msambatavangu , amewataka wanafunzi wanaomaliza masomo ya elimu ya juu kuanza kujiandaa na maisha yao sasa pasipo kuwa tegemezi.
Akizungumza na wahitimu wanaotarajiwa kupata shahada na stashada kutoka katika vitivo mbalimbali katika chuo kikuu cha Tumaini Iringa katika kongamano lililofanyika chuoni hapo siku moja kabla ya mahafali. Msambatavangu ameeleza kuhusu jinsi alivyoanza kazi ya ujasiriamali mpaka alipofikia kwa sasa.
“Nawaomba vijana wa kike na wakiume muelewe kuwa  maisha yenu ya sasa na baadae yanategemea sana jinsi ulivyojipanga na kutumia fursa mbalimbali haswa kupitia elimu uliyoipata katika kujiendeleza kimaisha "alisema.
Msambatavangu alisema mahali ilipofikia Tanzania kwa sasa kuhusiana na suala la ajira na kueleza kuwa pasipo kutumia fursa mbalimbali zilizopo wengi watabakia kulalamika kuwa hamna ajira na kufanya kuwepo kwa idadi kubwa ya wasomi ambao bado wapo katika umasikini mkubwa.
Mwenyekiti huyo alisema ana uhakika kama wanafunzi hao watatumia uwezo na maarifa waliyopata wakiwa chuoni hapo kwa vitendo watafanikiwa sana na kuwa waajiri wakubwa wa wengine na kuweza kupata maisha yaliyo bora. Na kueleza maisha bora hayaji hivihivi yamtaka kila mmoja kutumia fursa mbalimbali zilizopo kujiendeleza.
Katika kongamano hilo baadhi ya wanafunzi walifanya vizuri katika taaluma, michezo, nidhamu, uongozi bora na utunzaji wa mazingira, utafiti zilitolewa.
katika kitivo cha Uandishi wa habari waliofanya vizuri katika taaluma ni Elisha Magolanga, Bebi Kapenya na Fadhili Makenjula, Utafiti Lauson Mgani, Michezo Stella Munishi na Makenjula na Katika nidhamu Elisha Magolanga na Neema Malwala hao wakiwa ni baadhi katika vitivo vya taaluma mbalimbali vitolewavyo chuoni hapo.
Aidha mshauri wa kitivo cha Sayansi ya jamii na sanaa Profesa Seth Nyagava amewapongeza waliopata tuzo na kuwasihi wawe mabalozi wazuri waendako na kudhihirisha ubora wao.
Pia amewasihi wahitimu wote kuzingatia yale waliyojifunza wawapo kazini ili waweze kudumu kazini.
Mahafali ya 15 ya Chuo cha Tumaini yanatarajiwa kufanyika Jumamosi tarehe 27 Oktoba mwaka huu chuoni hapo.

No comments: