Monday, April 9, 2012

BONGE LA MECHI: Arsenal 1-0 Manchester City


Super strike: Arteta scores the winning goal
                           Mkwaju wa mbali wa Arteta umeipa ushindi Arsenal

Mkwaju wa mbali wa Mikel Arteta umeipa Arsenal ushindi muhimu na kuiacha Manchester City ikiwa pointi nane nyuma ya Manchester United katika ligi kuu ya England. 
 Out of control: Balotelli lunged in wildly on Alex Song
Yaya Toure alitoka mapema kutokana na kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na David Pizzaro huku Balotelli akitolewa kwa kadi nyekundu.
Mara mbili Robin Van Persie aligonga mwamba huku mkwaju mwingine aliopachika wavuni ukiwa wa kuotea.
 Getting in the way: Robin van Persie has an effort on goal that hits team-mate Thomas Vermaelen and goes over
Arteta alipata mwanya katika dakika ya 86 kwa kuachia mkwaju umbali wa yadi 25.
Jumping for joy: Arsenal fans do the Poznan celebration 
Mashabiki wa Arsenal wakishangilia


Arsenal walitawala kabisa Mechi hii na kukosa bao mbili za wazi na Man City walikuwa na wakati mbovu hasa yule ‘Toto Tundu’-‘Kwanini kila Siku mie’- Mario Balotelli akistahili kupewa Kadi Nyekundu mara 3 katika Kipindi cha Kwanza lakini akaambulia Kadi ya Njano na hatimaye kupata nyingine ya pili katika Dakika ya 89 na kutolewa kwa Kadi Nyekundu. Battle for the ball: Vermaelen collides with Manchester City's Sergio Aguero

Bao la ushindi kwa Arsenal, bao tamu sana, lilifungwa Dakika ya 86 na Mikel Arteta kwa kigongo cha mbali.

Vikosi vilivyoanza:

Arsenal: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta, Song, Walcott, Rosicky, Benayoun, van Persie

Akiba: Fabianski, Andre Santos, Oxlade-Chamberlain, Ramsey, Djourou, Jenkinson, Chamakh.

Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Lescott, Clichy, Toure Yaya, Barry, Milner, Aguero, Nasri, Balotelli

Akiba: Pantilimon, Richards, Pizarro, Dzeko, Kolarov, Tevez, De Jong.

Refa: Martin Atkinson






Arsenal sasa wamerejea katika nafasi ya tatu, pointi mbili juu ya Tottenham walio nafasi ya nne.
Time to go: Balotelli is sent off in the final minute
               
Nimekuvumilia sana toka nje sasa.... Mario Balotelli akipewa kadi nyekundu




All over? The Manchester City players look dejected at the final whistle 
Mwisho: Dakika 90 zikaisha Man city wakatoka kapa na huku wakiduwaa kama ligi imeisha.



[MECHI ZILIZOBAKI kwa Man United & Man City]
Man City Man Utd
Jumatano Aprili 11
Man City v West Brom
Jumamosi Aprili 14
Norwich v Man City
Jumapili Aprili 22
Wolves v Man City
Jumatatu Aprili 30
Man City v Man Utd
Jumamosi Mei 5
Newcastle v  Man City
Jumapili Mei 13
Man City v QPR
Jumatano Aprili 11
Wigan v Man United
Jumapili Aprili 15
Man United v Aston Villa
Jumapili Aprili 22
Man United  v Everton
Jumatatu Aprili 30
Man City v Man United
Jumamosi Mei 5
Man United v Swansea
Jumapili Mei 13
Sunderland v Man United
 

BONGE LA MECHI: Arsenal 1-0 Manchester City
Jumapili ya jana ya Pasaka katika uwanja wa Emirate kunawaka moto. Arsenal Ikiikaribisha Man City, huku kukiwa na taarifa kuwa Mancini hategemei kukaa muda mrefu Man City akiamini ameshaweka misingi ya Man City kushinda masimu ujao. Man City wakiwa nafasi ya Pili wakitazamia Ushindi kwao ndo muhimu zaidi ili kupunguza tofauti ya Pointi na Man United.
Arsenal nao ushindi kwao ni muhimu kujihakikishia wanashiriki UEFA mwaka huu.
Nani unadhani atashinda mchezo huu.? Maoni yako.

Timu Michezo GD Pointi

                                                                                                                                          
Man Utd
31 49 76
Man City 31 50 71
Tottenham
32 20 59
Arsenal 31 21 58
Chelsea 31 18 56
Newcastle 32 6 56

No comments: