Friday, May 11, 2012

Taasisi Ya Wakurugenzi Kuboresha Utendaji


Picha ya maktaba

 NA MAGRETH KINABO - MAELEZO
  10/05/2012

Makamu wa rais Dk. Mohamed Gharib Bilal  amesema kwamba Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania(IoDT) itasaidia kuboresha utendaji kazi kwa wakurugenzi wa taaasisi na mashirika mbalimbali  na  kuboresha utawala bora .

Aidha amewataka wananachi kuiunga mkono taasisi hiyo kwa kuwa ni chombo muhimu cha kikachosaidia kutoa mafunzo  kwa viongozi hao na kuwaunganisha  ili kuboresha utawala bora.

Kauli hiyo ilitolewa na Dk. Bilal wakati akizindua taasisi hiyo  leo (jana)  kwenye hafla iliyofanyika katika hoteli ya Haytt Regency jijini Dares Salaam.

“Taasisi hii itakuwa inawachukulia hatua baadhi ya wakurugenzi ambao hawatafuata maadili  na kanuni za IoDT ,ikiwemo kubadilishna mwazo na kupata uzoefu,” alisema Dk. Bilal.

Naye Mwenye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Wakurugenzi Tanzania(IoDT), Pius Maneno alisema  taasisi hiyo ina wanachama 19 ambao  kila mmoja amechangia sh. milioni 10 kwa ajili ya uanzishaji.

 Alisema lengo kuwa la  taasisi hiyo ni kutoa mafunzo  kwa ajili ya kuwajengea uwezo viongozi hao , kujenga mtandao na kuandaa mikutano mbalimbali.

 Katika uzinduzi huo , Profesa Geoffrey Mmari kutoka Chuo Kikuu cha Tuamini(TUDARG) na Mwenyekiti  wa African Life Assurance , Ibrahim  Mohamed  walitunikiwa cheti cha uanachama  wa  heshima.

No comments: