Saturday, July 28, 2012

YANGA FC WALAMBA BINGO DHIDI YA AZAM FC

Yanga leo ameweza kulaza chari mtanzania mwenzake katika fainali ya Kagame Cup ilisakatiwa katika Uwanja wa taifa  leo.
Azam Fc amelamba kichambo hicho cha 2-0 mara baada ya kuonesha uzembe wa kiufundi ulioweza kutumiwa vizuri na wapinzani wao kitu kilichopelekea kukubaliana  na hali iliyojili uwanjani hapo
Tutaendelea kukujuza zaidi......................

WACHEZAJI WA YANGA NA RAHA YA UBINGWA WA KAGAME CUP LEO

 Wachezaji wa timu ya Yanga wakishangilia na kombe lao walilokabidhiwa leo mara baada ya kuifunga timu ya Azam FC katika mchezo uliokuwa ni wa kuvutia kwa timu zote baada ya kuitandika timu ya Azam magoli 2-0 kwenye mchezo wa fainali katika michuano ya kombe la Kagame iliyomalizika leo kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Fullshangweblog na kikosi chake cha kazi inawapa hongera Wachezaji wa timu ya Yanga Uongozi na mashabiki wote wa Yanga pamoja na wanachama kwa kuutwaa ubingwa huo kwa mara ya pili mfurulizo hongereni sana.
 Wachezaji wa timu ya Azam ambayo imechukua nafasi ya pili wakipita jukwaani na kupewa medali zao baada ya mchezo huo kumalizika jioni ya leo kwenye uwanja wa Taifa.
Wachezaji wa timu ya Vita kutoka DRC Congo wakipta jukwaani na kupokea medali zao Vita wamechukua nafasi ya tau baada ya kuifunga timu ya APR ya Rwanda katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu uliofanyika kalba ya mchezo wa fainali.

No comments: