Saturday, October 13, 2012

Uharibifu Uliosababishwa Na Waislamu Mbagala.


 Mawe yametoboa vioo vingi
 Katika madhabahu, pameharibiwa

 Mabenchi yamepinduliwa na kuvunjwa
 Mimbari imechomwa na kuharibiwa



 Ofisi ya Kanisa imechomwa moto
 Wachungaji wa kanisa hili wakisubiria taarifa kutoka polisi
 Hawa wanafanya maombi na nimesikia wakiwaombea Waislamu Mungu awasamehe
 Vifaa vya uimbaji vimechomwa moto
 Washarika wakiwa kanisani kwao asubuhi hii
 Gari la mchungaji pia limeharibiwa kabisa

 Ofisi ya mchungaji na mwinjilisti zimeharibiwa kabisa
Kushoto ni msikiti walipotokea Waislamu kabla ya kuvamia kanisa kulia. Nyumba hizi za ibada ziko jirani zikitenganishwa na barabara tu

Askari wa jeshi la Polisi kikosi cha kutuliza ghasia wakiwadhibiti vijana waliokuwa wakileta vurugu eneo la mbagala kufuatia kijana mmoja anaesemekana anasoma kidato cha kwanza kukojolea mkojo Quraan na kusababisha hasira kwa waisilamu hassa vijana ambao walitapakaa mitaani na kuanza kuleta vuru.


Vijana waliosambaa mitaani na kuamsha vurugu kubwa kwenye eneo hilo la Mbagala Kizuiani.



Waisilamu waliotoka msikitini kwenye swala ya Ijumaa walikumbana na kimbembe cha kamatakamata hatakama hawakuwemo kwenye sakata hilo, alama ni kanzu na sijda





Hapa baadhi ya waisilamu walioamua liwalo naliwe nakuamua kuwatunishia msuli polisi nakusema pigeni mpendavyo hatoki mtu.





Barabara zilikua zikiharibiwa kwa moto ulikuwa ukiwashwa na waisilamu hao wenye hasira.


Maji ya kuwasha yalikuwepo ingawa hayakuweza kuzuia vurugu hizo.




Askari na watuhumiwa wakivuka pamoja kwenye mtaro wa maji taka.




Watuhumiwa wavurugu hizo wakipandishwa kwenye gari la polisi.
   Gari la  Kampuni ya…
  Baadhi ya waandamanaji wakiwa jirani na Kituo cha Polisi cha Maturubai kilichopo Mbagala jijini Dar leo.
    Baadhi ya maafisa wa polisi wakinawa maji baada ya mabomu ya machozi kupigwa.
   Gari la  Kampuni ya Clouds Media Group likiwa limepasuliwa kioo cha nyuma.
  Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Ally Ramadhani ambaye ni dereva wa daladala naye akiwa ameambulia kipigo baada ya kujichanganya na waandamanaji.
    …Dereva Ally Ramadhani akisikilizia maumivu.
     Mmoja wa waandamanaji.
     Baadhi ya waandamanaji wakiwa wamewekwa chini ya ulinzi.
Kanisa la Sabato Mbagala Kizuiani likiwa limevunjwa vioo.
…Vioo vilivyovunjwa kanisani hapo.
…kanisa hilo la Sabato.
  ...Muonekano wa kanisa hilo la Sabato.
    Jamaa aliyejitambulisha kwa jina la Paul Martin ambaye alidai alikuwa akienda sokoni ndipo akaambulia kipigo.
Kanisa la Aglikana ambalo pia lilishambuliwa na waandamanaji.
…Anglikana.
   Mabenchi ya kanisa la Anglikana yakiwa yametupwa nje.
Kibao cha kanisa kikiwa kimevunjwa.
  Muonekano wa kanisa hilo la Anglikana.
Gari lililokuwa ndani ya Kanisa la T.AG Mbagala Kizuiani likiwa limevunjwa vioo.
 
…Hili lilichomwa moto.
Baadhi wa waumini wa kanisa la T.A.G wakililinda kanisa lao.
---
WATU wanaodaiwa kuwa ni Waislamu wamevamia makanisa mbalimbali yaliyopo Mbagala Kizuiani jijini, Dar wakihamasisha vurugu wakimtuhumu mtoto Emmanuel Josephat kuwa amekojolea kitabu cha dini hiyo (Msaafu) Oktoba 10, mwaka huu.
Baadhi ya makanisa yaliyoshambuliwa ikiwa ni pamoja na kuchomwa moto magari yao ni  Kanisa la Sabato, Aglikana na T.AG .
(PICHA/HABARI: ERICK EVARIST/GPL)

No comments: