Wednesday, April 18, 2012

Bayern Munich yatisha kwa ukali wake


Real Madrid yafungwa na Bayern Munich

 
Bao lililofungwa katika dakika za mwisho na Mario Gomez iliiweka Bayern Munich kifua mbele kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya Real Madrid .

Ushindi huo ni katika duru ya kwanza ya mechi ya nusu fainali ya kombe la mabingwa bara ulaya.
Mshambulizi Franck Ribery alikuwa wa kwanza kuona lango la Real Madrid pale alipofumua mkwaju mkali na kumuacha kipa Iker Casillas akiwa hoi.
Lakini dakika sabu tu baada ya kipindi cha pili kuanza Mesut Ozil akiwa hauta chache toka langoni aliipatia bao lake.
Wengi walifikiri mechi hiyo huenda ikaishia kwa sare ya 1-1 kabla ya Gomez kuchafua mambo dakika za mwisho.
Kabla ya kufunga bao hilo Gomez alipoteza nafasi nyingi za kufunga.
Hata hivyo mwamba wa Real Madrid Cristiano Ronaldo hakua na siku njema kwani hakuna kubwa alilofanya akiwa uwanjani.

No comments: