Friday, April 20, 2012

Chu cha Splended chafanya mahafali ya ya 24 chuoni hapo

Mkuu wa chuo cha Uhalizi pamoja na ualimu Splended kilichopo Ilala jijini Dar es Salaam bwana  Cassim Taalib akihutubia wakati wa mahafali ya 24 ya chuo hicho yaliyofanyika leo hii katika chuo hicho jijini Dar es Salaam.
(PICHA ZOTE NA PHILEMON SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Aliyekuwa mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Tabora mstaafu bwana Abedi Mwinyimusa ambaye ndiye mgeni rasmi katika mahafali hayo akihutubia wanafunzi pamoja na wazazi waliokuwemo katiaka mahafali hayo ambapo aliwataka wanafunzi kuwa na juhudi pindi wawapo kazini na pia kuwa na nidhamu kazini.
Edda willbert(kushoto) na Havilla Helbert ambao ni wahitimu katika mafunzo yao wakisoma risala ambapo walimtaka mgeni rasmi awasaidie kupata vifaa vya kujifunzia ambapo walivyonavyo kwa sasa vimechakaa.
Mgeni rasmi ambaye ni Abedi Mwinyimusa(kulia) pamoja na mkurugenzi wa chuo Cassim Taalib wakiingia ukumbini.
)Kikundi cha ngoma maarufu kama Safi Theater kikitoa burudani katika mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu wakifurahia siku hiyo ambayo ni historia katika maishayao.
Baadhi ya wazazi wa wahitimu waliohudhuria katika mahafali hayo.
Mgeni rasmi pamoja na Mkurugenzi wa chuo wakifurahia burudani iliyotolewa na kikundi cha Safi theater.
Mgeni rasmi ambaye ni Abedi Mwinyimusa pamoja na mkurugenzi wa chuo Cassim Taalib wakiwa kwenye picha ya pamoja na wahitimu.

No comments: