Friday, April 20, 2012

WENYEVITI WA KAMATI ZA BUNGE ZA FEDHA ZA UMMA WAKUTANA NA KATIBU MKUU KIONGOZI, BUNGENI DODOMA

Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue (Kulia) akimsikiliza mwenyekiti wa kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe. John Cheyo (katikati) wakati alipofanya ziara ya kikazi Bungeni Dodoma. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Zainabu Vulu. Balozi Sefua alifanya ziara ya kikazi Bungeni kwa lengo la kujitambulisha 
Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue (Kulia) akimsikiliza makamu mwenyekiti wa kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma  (POAC) Mhe. Deo Filikunjombe wakati alipofanya ziara ya kikazi Bungeni Dodoma. Katikati  ni Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Zitto Kabwe. Balozi Sefua alifanya ziara ya kikazi Bungeni kwa lengo la kujitambulisha
. Katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue (Kulia) akizungumza na mwenyekiti wa kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) Mhe. Agustino Mrema wakati alipofanya ziara ya kikazi Bungeni Dodoma. Kushoto  ni Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Idd Azzan. Balozi Sefua alifanya ziara ya kikazi Bungeni kwa lengo la kujitambulisha

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya katibu wa Bunge Bungeni Dodoma. Balozi Sefua alifanya ziara ya kikazi Bungeni kwa lengo la kujitambulisha kwa viongozi mbalimbali wa Bunge.
 Katibu wa Bunge  Dkt. Thomas Kashililah akiwa katika mazungumzo na katibu Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue, wakati Balozi Sefue alipofanya ziara ya kikazi Bungeni Dodoma. Kushoto ni Msaidizi wa Katibu wa Bunge Nd. Emmanuel Mpanda, pamoja na Mkurugenzi wa Shughuli za Bunge Ndg. John Joel.

Katibu wa Bunge  Dkt. Thomas Kashililah akimkabidhi Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue vitabu vya orodha ya Wabunge pamoja na kanuni za kudumu za Bunge wakati alipofanya ziara ya kikazi Bungeni Dodoma.

No comments: