
  Taarifa za hivi punde kutoka Bungeni Mjini Dodoma,zinaeleza kuwa  Kusudio la Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe la kutaka  kupiga kura za kuanzishwa kwa mjadala wa kutokuwa na imani na Waziri  Mkuu,Mh. Mizengo Pinda,limepigwa chini na Spika wa Bunge,Mh. Anne  Makinda.
Akisoma  kanuni za Bunge,Mh. Spika alisema kwa mujibu wa kanuni za Bunge na  Katiba ya Nchi,kusudio la kutaka kumuondoa Madarakani Waziri Mkuu kwa  kupiga kura ya kutokuwa na Imani nae ambayo ni taarifa ya maandishi  inapaswa kuwasilishwa kwake siku 14 kabla ya siku husika.
Hivyo  kwakuwa ofisi yake haijapata taarifa ya maandishi ju ya zoezi hilo,basi  zoezi hilo moja kwa moja litakuwa ni batili, na kwasababu kikao hicho  cha Bunge kinatarajiwa kufungwa siku ya jumatatu,basi hakutakuwa na  uwezekano wa zoezi hilo kukamilika.
Awali  Mbunge wa Jimbo la Bumbuli,Mh. January Makamab aliomba muongozo wa  Spika kuhusu jambo hilo ndipo Spika,Mh. Anne Makinda akasimama na kutoa  ufafanuzi huo
 
 
No comments:
Post a Comment