Sunday, November 25, 2012

LEOKATIKA MTAZAMO WA MJENGWA

Makubwa Haya;Jengo Lajengwa Mtwara Jiwe La Msingi Lawekwa Dar

 Habari ya jumapili ndugu zangu, ni matumaini yangu siku imeanza vyema ila poleni kwa wote ambao siku ya leo haijanza vizuri kwao ila naamini itaisha vizuri kwao.
Leo nimewasili majira ya saa mbili mkoani mtwara nikitokea Jijini Dar kikubwa ambacho  nimekiona katika mkoa huu ni mandahari ya kuvutia ya uwanja wa ndege ambao sehemu kubwa ya jengo la uwanja limekarabatiwa ,sina budi kuwapa sifa mamlaka zinazohusika na viwanha vya ndege kwa kazi nzuri na ni wito wangu kazi ya ukarabati iendelee na kwa viwanja vingine pia.
Nikiwa bado nashangaa mjini wa mtwara, niliweza kumuuliza maswali wawili matatu mwenyeji wangu kuhusu historia ya mkoa huu ukiachilia mbali yale ninayoyafahamu ambayo nimesoma kwenye Somo la jiografia nikiwa shule.
Swali kubwa lilikuwa kwanini  watu wa mikoa ya kusini wamekuwa wakilalamika kuwa wametengwa na shughuli za kimaendeleo, mfano miundombinu nk, jibu likikuwa jepesi sana mwenyeji wangu aliniambia Historia ndio inayofanya mikoa hii kuwa nyuma aliweza kuniambia mengi kuhusu historia.
Swali hili linipa jibu ambalo sikutegemea kulisikia ila lilinistua na kunifanya nisahau kuuliza kwa undani je ni historia ipi iliyoitenga mikoa ya Kusini na maendeleo nikajikuta naama nje ya mada, na kudadadisi kitu kingine na swali lilikuwa hivi, JE GAS IMEINUFAISHA VIPI MKOA HUU?, hapa ni kama niliweka chumvi kwenye kidonda kibichi,  jibu lilikuwa gas imekuwa kilio cha wananchi wa eneo ili maana walitegemea miaka yote waliyosaauliwa katika maendeleo baada ya eneo lao kutumika uwanja wa mapambano wakati ukombozi kusini mwa bara la africa hasa nchi za Msumbiji,zimbabwe, labda gas hiyo ingeziba matundu ya simanzi yaliyopo mioyoni mwao labda gas ingekuwa fidia ya kucheleweshewa fursa za maendeleo.
Hayo ni maswali ambayo wananchi wa kusini wamekosa majibu ya kuwaridhisha leo hii wanahoji iweje Rais azindue mradi wa Gas jijini dar wakati Gas ipo mtwara, ni kufikia kutoa mfano ni sawa jengo linajengwa Mtwara kisha Jiwe la Msingi linaweka Dar  hapa wananchi wanahisi hatua hii itazidi kuchelewesha maendeleo zaidi katika mkoa wao maana wanahoji kama gas itakuwa ianpatikana dar je wawekezaji wataona umuhimu gani wa kuja kuwekeza Mtwara?
 
Binafsi sipendi kuwa jaji katika jambo hili kuhukumu kama nia ya serikari ni mbaya au la  labda wananchi wanaona wamesalitiwa wanatamani hiki walichobarikiwa na Mungu kiwatoe katika hali ya umasikini nadhani hii ni fursa sasa ya serikari kuona ni namna gani wananchi wa maeneo haya hawapotezi imani na Serikari ya , yapo mambo muhimu serikari inaweza kufanya ili wananchi hawa wasizidi kusononeka zaidi mi nashauri kama yawekena hata kama Gas itasafirishwa kwenda popote ila nadhani wananchi wa maeneo haya wangepewa kipaumbea maana tunaambia Gas inakwenda kuzalisha umeme hivyo nadhani wananchi wa mikoa ya kusini wangefikiriwa hata kupunguziwa gharama ya  nishati ya umeme kwangu mimi hii naona itakuwa moja ya jawabu .
Huu ni mtazamo wangu kama mtanzania

No comments: