Sunday, November 25, 2012

SAJUKI KUWASHUKRU WATANZANIA UWANJA WA SAMORA IRINGA LEO

Juma Kilowoko

Sajuki msanii wa filamu Swahiliwood kufunika Iringa kwa Show kali.
Juma Kilowoko
Sajuki akiwa makini kupitia mistari ya wimbo.
Juma Kilowoko
Sajuki akiwa na mkewe Stara Studio.
Wastara Juma
Stara mke wa Sajuki akiandika mistari.
JUma Kilowoko
Sajuki

KATIKA kutoa shukrani kwa Watanzania wote waliowajibika katika kuhakikisha wanamsaidia mwigizaji na mtayarishaji mahiri wa filamu kutoka Swahiliwood Juma Kilowoko ‘Sajuki’ kupatiwa matibabu kutokana na maradhi ya tumbo na kwenda kutibiwa Nchini India na kupona, kampuni ya Wajey Film Company imeandaa tamasha kubwa la shukrani.

Wastara Juma ‘Stara’ amesema kuwa baada ya mumewe Sajuki kupata matibabu anatumia fursa hiyo katika kuwashukru watanzania waliojitoa kwa hali na mali katika kufanikisha matibabu hayo.

“Sisi kama familia hatuna cha kuwalipa watanzania kwa moyo wao wa upendo walioonyesha kwetu, katika kipindi kigumu na majaribu wakati Sajuki akiwa anaugua, si rahisi kumfikia kila mtu kwa wakati mmoja lakini kwa njia ya tamasha hilo tutawafikia, tunawapenda watanzania mungu awabariki sana,”anasema Stara.

Tamasha hilo linatarajia kufanyika leo  jumapili tarehe 25/11/2012 katika uwanja wa Samora huku wasanii wa muziki wakitumbuiza kwa nguvu Mzee Yusuf, Linah, H. Baba na mchekeshaji Kitale ataimba burudani kubwa ni pale mechi kali itakapopigwa kati ya wasanii nyota wa filamu kutoka Bongo movie na timu kali ya watangazaji wa redio zote mkoani Iringa.

Ni Tamasha la aina yake kila mwairinga anatakiwa asilikose kwani ni tamasha la kipekee kufanyika Iringa, pia Stara alisema onyesho hilo litafanyika kwa ajili ya kukusanya fedha zitakazopelekwa kwa wasanii wanaosumbuliwa na maradhi na kukosa matibabu alisisitiza mratibu huyo.

Baada ya  mechi burudani  itahamia   ukumbi  wa club V.I.P kwa  kiingilio cha Tsh 3000 na uwanjani  kiingilio ni buku tatu tu 

No comments: