Tuesday, May 8, 2012

KAMPUNI YA SEMES YAJIDHATITI KUKOMBOA WANAWAKE MKOANI ARUSHA


Meneja masoko wa SEMES  Atupele Elias akionyesha moja ya mashine za kufanyia usafi katika ofisi mbalimbali na numba mjini Arusha.
Baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya SEMES wakiwa katika picha ya pamoja.
NA GLADNESS MUSHI WA FULLSHANGWE-ARUSHA

KAMPUNI ya Semes ya jijini la Arusha imeweka mikakati ya kuhakikisha kuwa  inawaakomboa wanamke wa nchi ya Tanzania  kwa kuwapa elimu ya ujasiriamali sanjari  na kuwapatia mitaji ili iwawezeshe kujikwamua kiuchumi.

Hayo yalisemwa na mkurugenzi wa kampuni hiyo Bw Elias Seme alipokuwa katika sherehe za kuzindua kikundi cha kampuni hiyo jijini hapa

Alisema kuwa ili kuhakikisha kuwa wanawake wanaondokana na hali ya utegemezi kampuni hiyo imejipanga kuhakikisha kuwa wanawake wanapewa kipaumbele katika kuwakomboa kwa kuwapatia mitaji mbali mbali .

Alieleza kuwa mwanamke ndie mwenye huruma na ana uwezo wa kupangilia mipango zaidi ya wanaume hivyo wanayo fursa kubwa ya kuwezeshwa ili waweze kujikwamua kiuchumi

Bw Seme aliongeza kuwa kampuni hiyo tayari.imeshatoa mitaji ya shilingi milioni tano kwa mwaka huu ambapo pia wameweza kuanzisha vikoba kwa  lengo la kukopeshana ili kuboresha maisha yao

Aliongeza kuwa mbali na hayo kampuni hiyo imefanikiwa  kutoa ajira kwa vijana 21 ambapo  lengo halisi ni kuweza kutoa ajira kwa watu 50-60 kwa mwaka .

Akielezea changamoto inayoikabili kampuni hiyo alisema kuwa ni pamoja na ushindani wa kibiashara ambapo kumekuwepo na makampuni mengi kutoka nchi ya nje  yanayohusiana na maswala ya  usafi hivyo kuwepo na upinzani    mkubwa.

Alitaja mikakati waliyonayo kuwa ni pamoja na kuongeza vitega uchumi zaidi na kujiboresha ili iweze kujiongezea mapato zaidi ili kuwawezesha vijana wengi kujipatia ajira.

No comments: