Monday, May 7, 2012

KIJANA ADAIWA KUUWAWA NA WANANCHI WENYE HASIRA KALI

Kisa ni kibaka

 Leo asubuhi maeneo ya chuo kikuu cha Dar es salaam kitivo cha Elimu DUCE mkabala na Kambi ya Jeshi la Kujenga Taifa JKT Mgulani katika barabara ya Chang'ombe Camera ya Fullshangwe imenasa tukio la kibaka huyu ambaye amekutwa akiwa ameuwawa huku tairi likiwa linawake pembeni. inasadikiwa alikutwa katika nyumba za jirani na eneo hilo akitaka kuiba hivyo wananchi wenye hasira kali wakamkamata na kumpiga na kuchoma tairi ili kumuunguza, hata hivyo haijulikani nani alimuokoa asiungue na tairi hilo japokuwa amepoteza maisha
Wanafunzi wakiushangaa mwili wa kibaka huyo aliyepigwa na wananchi wenye hasira na kuuwawa wakati akitaka kuiba katika moja ya  nyumba kwenye eneo hilo.

No comments: