Tuesday, May 1, 2012

SHEREHE ZA WAFANYAKAZI MEI MOSI MKOANI DAR ES SALAAM LEO

Kaimu mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bi Mwnantum Mahiza akitoa hotuba wakati wa sherehe za MEI MOSI leo zilofanyika katika viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dar es salaam ambapo kitaifa sherehe hizo zimefanyikia mkoani Tanga mgeni rasmi akiwa Rais  wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Jakaya Kikwete.Kushoto ni Mwenyekiti wa TUCTA mkoa wa Dar es salaam Bw Hassan Kaumo.
(PICHA NA PHILEMN SOLOMON WA FULLSHANGWE)
Wafanyakazi kutoka Vyama mbalimbali vya wafanyakazi wakiwa wamefurika katika viwanja vya mnazi mmoja kusherekea MEI MOSI leo huku watu wengine wakijaribu kuingia katika viwanja hivyo kama wanavyoonekana katika uzio.
 Baadhi ya wafanyakazi wakiwa katika viwanja vya Mnazi Mmoja wakisubiri kuanza kwa sherehe hizo jijini Dar es salaam.
Unaweza ukafikiria huyu ni mlemavu Lah. siyo mlemavu ila kijana huyu aliyetambulika kwa jina la Hashimu Ibrahimu aliamua kutoa burudani kwenye sherehe za Mei Mosi ili kujipatia kipato.kama usemi unaosemwa mgeni njoo mwenyeji apone.

No comments: