Thursday, November 22, 2012

MTOTO JULIANA MWINUKA ANAENDELEA VIZURI.


Hali ya sasa ya mtoto Juliana baada ya kufanyiwa matibabu ya awali


Mtoto Juliana Mwinuka
Majeraha  yaliyotokana na kuungua moto klatika  uso wa mtoto  mtoto  Juliana Mwinuka (16) mkazi  wa kitongoji cha Ushindi kata ya Mavanga  wilaya ya  Ludewa  mkoa  wa Njombe yameanza kuziba taratibu huku akiwa amefanyiwa oparesheni zaidi ya wiki mbili  sasa katika Hospitali ya CCBRT.


Kwa sasa anaendelea  vizuri na sura yake imeanza kurudia katika hali ya kawaida japo bado kufanyiwa  oparesheni nyingine .

 Mtandao huu unaendelea kuwapongeza wote wanaoendelea kuguswa na kuungana na wadau wengine kumchangia fedha za matibabu ,mtoto Juliana kama anavyoonekana akiwa ameunga uso wake kwa moto ni yatima anahitaji msaada wako ili kunusuru maisha yake waweza kutuma mchango wako kwa njia ya M-PESA katika namba hii 0754 026 299 au Tigo Pesa 0712 750199 namba hizi ni za mmiliki wa mtandao huu Bw Francis Godwin

Nawaomba tuungane kufanikisha kuokoa maisha ya mtoto Juliana Mwinuka na Mungu atatuongezea zaidi

No comments: