Monday, September 24, 2012

HIZI NDIO MBINU ZILIMFANYA RAMIRES AIMUDU LIGI NGUMU YA ENGLAND

Pamoja na kuwa na umbo dogo mchezaji wa Chelsea Ramires amekuwa ni mmoja ya wachezaji wachache wageni waliofanikiwa kuupatia mchezo wa ligi kuu ya kiingereza ndani ya kipindi cha muda mfupi aliokaa na timu hiyo. Anaonekana ni mchezaji mapafu ya mbwa, mwenye kujituma vilivyo kwa ajili ya kuipigania timu yake, pamoja na kuwa na mwili mdogo Ramires amekuwa na uwezo wa kupambana na mijitu iliyoshiba inayocheza kwa nguvu kwenye ligi kuu ya England. Amewezaje kuweza kuimudu vizuri EPL? Ramires anaelezea mbinu zake.

1: CHEZA KIBABE
Nilipofika England kwa mara ya kwanza. Nilikuwa nikicheza nadondoka kila mara na nikagundua kwamba mashabiki walikuwa wanachukizwa na jambo lile. Lakini sikuwa najiangusha , bali nilikuwa sijazoea ile hali ya mchezo wa kiingereza. Kama unavyoniona sina nguvu sana, hivyo nikagundua ili kuwatisha wapinzani wangu inabidi nicheze kibabe. Baadae nikagundua haisadii sana kwa sababu inakuwa kama unaanzisha ugomvi. Kama ukicheza kibabe na yeye atakurudishia na hali itaendelea mpaka mwisho, lakini inasaidia kuwaonyesha kwamba japokuwa una mwili mdogo hawawezi wakakuonea kwenye kupambana dimbani.


2: JARIBU KUTOKUWA NAO KARIBU WAPINZANI 
Kama ambavyo naitumbua sina nguvu sana, ikiwa nitapokea mpira huku mpinzani wangu akiwa nyuma yangu nitajitahidi kadri niwezavyo kutoa pasi mapema iwezekanavyo.  Najaribu kuzuia kucheza huku mgongo wangu ukiangalia nyuma kwenye goli - kwasababu ni bora zaidi kucheza huku ukiwa unatazamana na mpinzani wako.
Ikiwa nahitajika kufanya marking kwa mchezaji ambaye ana nguvu kuniliko, nafahamu kwamba ni vizuri kutokalibiana nae na kujaribu kutumia mikono yangu, vinginevyo atanikumba. Hivyo najaribu kuwapa nafasi na kusubiri muda muafaka kumuingia kwa kushtukiza.  Siwezi kushindana nao kwa nguvu, hivyo natumia wepesi wangu kama njia mbadala ya kuwashinda.

3: KULA CHAKULA VIZURI NA KUPUMZIKA VYA KUTOSHA
Lishe bora na mapumziko ni muhimu sana katika kuwa na nguvu. Kabla ya mechi mara zote huwa nakula tambi, samaki au kuku, na siku moja kabla ya mechi na siku ya mechi huwa nakunywa maji mengi kuliko kawaida. Hii imekuwa tabia yangu kwa muda mrfu sana na kuna baadhi ya wachezaji wenzangu wananitania sana kuhusu hili, lakini siku zote imekuwa inanisaidia na najihisi kujiamini sana, hivyo kwanini nibadilishe mfumo huu au nibadilishe diet yangu? Baada ya mazoezi, naenda moja kwa moja nyumbani kupumzika vya kutosha, muda mwingine nikijifurahisha na video games au kuangalia filamu. Hili jambo ni muhimu sana kwangu, na lazima kila siku ya mungu nilale kwa muda wa masaa yasiyopungua nane."

No comments: