Wednesday, September 12, 2012

KOSA MOJA GORI MIA (KIFO CHA DAUDI MWANGOSI CHALETA MATUMAINI MAPYA KWA WANAHABARI)



Wanahabari wakimsikiliza Mwenyekiti wa klabu wa waandishi kagera baada ya kupokea maandamano ya amani ya kupinga mauaji ya aliyekuwa mwandishi wa channel ten Daudi Mwangosi

Askari wa usalama barabarani akiongoza maandamo ya waandishi wa habari mkoa wa Kagera
Wanahabri wa mkoani kagera leo kwa pamoja wameungana na wenzao nchi nzima katika maandamano ya amani ili kuweza kukemea vilivyo vitendo vya kikatili vinavyoendelea hapa nchini Tanzania kupitia vyombo vya usalama wa raia.
Wakiongea katika wakati tofauti wamesema kwa kipidi kirefu sana wamekuwa wakikutana na mazingira magumu katika kazi zao, hivi sasa wanahitaji kuheshimiwa kama wanajamii na kama watanzania wengi.

Pia wengine wamesema kuwa kwa ujumla mauaji ya kikatili juu ya mwandishi mwenzao yaliyotokea hivi karibuni kuwa yamewahakikishia kuwa hawalindi na vyombo vya usalama bali wanjilinda wao wenyewe , kutokana na hali hiyo wanaiomba serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania kuwachukulia hatua za kisheria wale wote waliohusika na mauaji hayo.

Tunaendelea .......................

No comments: