Friday, November 30, 2012

MADIWANI MANISPAA YA IRINGA NA ILALA WADAIWA KUDANGANYWA KIWANDAN.

 Haya ni mazingira ya  kiwanda cha  Dabaga  ambayo yanaongoza kwa  kuwa harufu kali kutokana na uchafu

Zikiwa  zimepita siku chache toka madiwani  wa Halmashauri ya Ilala jijini Dar es Salaam na wale wa  Manispaa ya Iringa  kufanya  ziara  katika kiwanda cha Dabaga Vegetable kilichopo Ipogolo na  kuvutiwa na hali ya  usafi  wa kiwanda  hicho  , wafanyakazi wa  kiwanda hicho  wafichua siri wadai madiwani  walidanganywa juu ya usafi.

 Wakizungumza na mtandao  huu wa www.francisgodwin.blogspot.com wafanyakazi wa  kiwanda hicho ambao  waliomba majina yao kuhifadhiwa  kwa usalama  wao  ,walidai kuwa  wakati wa  ziara ya madiwani hao  uongozi  wa kiwanda  hicho  ulilazimika  kufunga  kiwanda  kwa  muda ili  kupisha  ziara  hiyo kutokana na mazingira ya  kiwanda hicho  kuwa machafu.

Kwani  walisema  kuwa kwa kawaida  mazingira ya  kiwanda  hicho ni machafu  zaidi na kuna haja ya  viongozi hao  wakiwemo madiwani  wa Manispaa ya Iringa  kujenga utamaduni wa  kufanya ziara za ghafla katika  viwanda  hivyo  ili  kuona hali halisi badala ya  kufanya ziara  zenye taarifa kama hiyo  iliyofanyika na kupelekea  uongozi wa kiwanda hicho  kujiandaa kwa usafi zaidi.


Wafanyakazi hao  walisema harufu mbaya ya uchafu iliyomo ndani ya kiwanda hicho hata  wao wafanyakazi  imekuwa ikiwaweka katika  wakati mgumu  ila madiwani walikubali  kudanganywa kwa zawadi ndogo ndogo  walizopewa  wakati wa ziara  hiyo na kuwa kuna haja ya madiwani hao hasa kamati ya afya  na mazingira  kufika  kufanya ukaguzi  katika  kiwanda hicho na viwanda vingine mjini Iringa .

No comments: