Gari la kifaharia alilokuja nalo mutumiwa mahakamani
Kwa mara ya kwanza jeshi la Police Tanzania limetampeleka mtuhumiwa wa mauaji ya mwandishi wa habari Mwangosi kizimbani.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi amesema askarianayetuhumiwa kusababisha kifo cha aliyekuwa mwandishi wa habari wa kituo chatelevisheni cha Channel 10, marehemu Daudi Mwangosi amefikishwa mahakamani leo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara hiyo iliyosainiwa na Waziri Nchimbiilieleza kwamba Septemba 7,mwaka huu alikabidhiwa taarifa ya awali ya uchunguziwa polisi juu ya kifo cha mwandishi huyo na Mkuu wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali Said Mwema.Hivyo Septemba 11, mwaka huu aliliagiza Jeshi la Polisi kumpeleka mtuhumiwa huyoaskari namba G. 2573 PC Pasifious mahakamani leo kama ilivyotakiwa maMkurugenzi wa Mshtaka(DPP). Waziri Nchimbi alisema wakati mtuhumiwa huyo amefikishwa mahakamani , kamatiiliyoundwa chini ya Jaji Ihema itaendelea na kazi yake ili kupata suluhisho lakudumu la migongano ya kikazi kati ya polisi na waandishi wa habari na waandishi wahabari, polisi na vyama vya siasa ikiwemo kuboresha mahusiano zaidi kati ya polisina raia. Aliongeza kuwa mkondo wa sheria umeanza kufuatwa nawaomba wadau wote kutoa nafasi kwa utaratibu huo wa kisheria kufanya kazi.Aidha aliongeza kuwa uchunguzi huo wa awali ulibaini mambo makubwa mawili ,ambayoni mlipuko uliotokea ulitokana na bomu la Machozi na bomu hilo lilifyatuliwa naaskari huyo.



No comments:
Post a Comment